'DAWA YA DENGUE SI MAJANI YA MPAPAI'...MWANANCHI WAONYWA WASIFUATE UDANGANYIFU HUO WA WAGANGA WA JADI....

Sunday, May 18, 20140 comments


Halmashauri  ya  manispaa  ya  Ilala  imesema  kuwa  majani  ya  mapapai  si  tiba  ya  ugonjwa  wa  dengue  hivyo  ni vyema  wananchi wakafika  hospitalini  kupatiwa  dawa  kuliko  kudanganywa  na  waganga  wa  jadi....

Kauli  hiyo  ilitolewa  Dar es Salaam jana  na  kaimu  mganga  mkuu  wa  manispaa  ya  Ilala, Dr  Willy Sango, wakati  wakitoa  mafunzo  kwa  wenyeviti  wa  serikali  za  mitaa  jinsi  ya  kuelimisha  wananchi  jinsi  ya  kujikinga  na  homa  ya  dengue...

Dr Sango  alisema  ugonjwa  wa  dengue  hauna  tiba  wala  chanjo  bali  wanatibu  dalili  za  ugonjwa  huo  tu, hivyo  ni  vyema  wananchi  wakachukua  tahadhari  ya  kujikinga  nao....

Pia  aliwataka  waganga  wa  jadi kuacha  kuwadanganya  wananchi  kwa  kusema  kuwa  majani  ya  papai  yanatibu  kwani hiyo  si  kweli  na  hayajathibitishwa  na  wataalam  wa  afya...

Alisema  kuwa  mtu  akiugua  anatakiwa  aende  hospitali  kwanza, asiende  kutumia  dawa  bila  kupima  kwani  hiyo  ni  hatari, hivyo  wananchi  wanatakiwa  kufika  hospitalini  kupima  ndipo  waanze  kutumia  dawa....

Hata  hivyo  alisema, wenyeviti  wa  serikali  za mitaa  wanatakiwa  kuhakikisha  wanasimamia  vizuri  maeneo  yao  pamoja  na  kushauri  wananchi  kwenda  hospitali  na  kuacha  kudanganywa  na  majani  ya  mapapai....

"Majani  ya  papai  si  dawa  ya  dengue  wala  hayajathibitishwa  na  mpaka  sasa  hakuna  dawa  ya  ugonjwa  huo. Tunacho tibu  ni  dalili  zake  tu, hivyo  wananchi  msidanganyike  na  waganga  wachache  wanaotaka  pesa," alisema  Dr  Sango

Pia  alisema  kuanzia  kesho, dawa  zitaanza  kupuliziwa  mtaa  mmoja  baada  ya  mwingine  ili  kuua  mazalia  ya  mbu  hao  wanaoeneza  ugonjwa  huo....

Hata  hivyo  alisema  kuwa  watu  wanaopulizia  dawa  hizo  wanatakiwa  kufika  katika  ofisi  za  serikali  za  mitaa  ili  watambuliwe  kwanza  ndipo  waendelee  na  zoezi  hilo.
Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. NDANI YA JAMII - All Rights Reserved