TUKIO LINGINE LA KIGAIDI LAIOMA ZAIDITIKISA KENYA LEO....SOMA ZAIDI

Tuesday, March 25, 20140 comments



Baada ya tukio la Westgate ambalo lilichukua maisha ya watu wengi, jiji la Nairobi limekumbwa na tishio jingine la aina hiyo kwenye eneo la biashara la Nakumatt Junction Barabara ya Ngong ambapo yamekutwa masanduku manne ya kubebea risasi kwenye eneo la kuegesha magari kwenye vyumba vya chini (Basement). 

Masanduku hayo yalipatikana ndani ya toroli la kubebea mzigo kutoka kwenye duka la jumla la Nakumatt ambapo walioshuhudia wamesema sanduku hizo zilikuwa zimeandikwa ‘explosion’ na walipoitwa wataalam wa mabomu  wakagundua kuwa sanduku ni za kubebea milimita 9 risasi za bunduki aina ya ceska ama Mp5 machine gun.
 
Masanduku hayo yaligundulika wakati wafanyakazi wakirudisha matoroli hayo ndani baada ya wateja kuyatumia na kuyaacha eneo la parking.
Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. NDANI YA JAMII - All Rights Reserved