ANT LULU AIBIWA NGUO ZA NDANI...ATOA ONYO KWA KURIPOTI KWA MTAALAMU WAKE BAGAMOYO

Wednesday, October 16, 20130 comments


MSANII wa filamu za Kibongo aliyeibukia kwenye utangazaji, Lulu Semagongo ‘Aunty Lulu’ amekombwa vitu kibao vya thamani dukani kwake na watu wasiojulikana.

Tukio hilo la kuhuzunisha lilitokea wiki iliyopita, usiku wa manane katika duka la msanii huyo lililopo  Kinondoni – Biafra jijini Dar es Salaam ambapo vitu vilivyoibwa ni pamoja na Chupi zake,  viatu, nguo, pochi, simu na fedha.
 

“Kwa kweli nimechanganyikiwa sana, hadi sasa bado sijajua thamani ya vitu vyote kwa jumla ni kiasi gani lakini nasema sitaki lawama. Walioniibia ni heri wanirudishie tu kwa njia yoyote maana kitakachowakuta hawatasahau.
 

“Nimeshakwenda Bagamoyo kwa mtaalamu wangu na kazi imeshakwisha. Natoa siku saba vitu vyangu viwe vimerudi vinginevyo...” alisema Aunty Lulu bila kufafanua zaidi

Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. NDANI YA JAMII - All Rights Reserved